Pages

Subscribe:

Sunday, December 31, 2017

HAMISA MOBETO AAMUA KUWA SINGLE NA KUWAACHA ZARI NA DIAMOND WAENDELEE

Hivi karibuni kumekuwa na maneno mengi sana kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana ishu nzima ya Zari na hamisa kurushiana vijembe kwenye mitandao ya kijamii kisa kikidaiwa ni Diamond.

Ambapo kila mtu ameonyesha kusema ya kwake kwa upande wake na kutafsiriwa tofauti na vitu kama hivyo na mwisho wa siku watu wakatafsiri kuwa Diamond yupo upande wa Zari though alimkosea...
na Zari kuonekana kumsamehe Diamond na kuwa pamoja hadi sasa, hivyo muendelezo wa vijembe vya Zari na Hamisa vilikuwa vinatafsirika kama kumgombea Diamond.

Kupitia snapchat account ya Hamisa amepost maneno yanayosema nani yupo tayari kuingia mwaka 2018 akiwa single yaani bila mwanaume, post hiyo imetafsirika kama Hamisa amekubali kuendelea na maisha mapya 2018 bila kuwa na mahusiano na diamond ni kama amekubali yaishe tu.

Kwani Diamond ameamua kuwa na Zari jumla, kama ufahamu tu Hamisa na Diamond wamezaa mtoto mmoja wa kiume kwa upande wa Hamisa anamuita Abdulatif na Diamond anamuita Dylan.

0 comments:

Post a Comment