Pages

Subscribe:

Sunday, December 24, 2017

UFUGAJI WA MBWA UNAPUNGUZA VIFO KWA 36% KWA WAGONJWA WA MOYO

Utafiti uliofanywa na wanasayansi nchini Sweden unaonesha kuwa watu wanaofuga mbwa hupunguza hatari ya kifo kutokana na magonjwa ya moyo.

Utafiti huo unaonesha kuwa kufuga mbwa hupunguza kwa asilimia 36 hatari ya kifo kwa wenye magonjwa ya moyo hususani kwa wanaoishi peke yao, Kwenye nyumba ambazo huishi watu wengi, mbwa huwa hawana...
athari hii moja kwa moja lakini huweza pia kupunguza vifo hivyo vya magonjwa ya moyo kwa asilimia 15 tofauti na watu wanaoishi peke yao wakiwa wanafuga mbwa.
 
Hatahivyo utafiti huu haujaeleza moja kwa moja kwanini mbwa wanaweza kusababisha manufaa haya lakini imeonesha kuwa watu wanaofuga mbwa huishi maisha ya afya zaidi ya wasiofuga mbwa.

0 comments:

Post a Comment