Pages

Subscribe:

Wednesday, November 15, 2017

MUME WA ZAMANI WA IRENE UWOYA (MZAZI MWENZIE) NDIKUMANA AFARIKI DUNIA



Habari ya kusikitisha, mume wa zamani za Irene Uwoya, Ndikumana Hamad Katauti amefariki dunia. 

Alikuwa kocha msaidizi wa timu ya soka ya Rayon Sports ambayo inaongoza kwa kuwa na mashabiki wengi nchini Rwanda. Uongozi wa timu hiyo umesema jana Katauti alifanya mazoezi na wachezaji wake akiwa...
buheri wa afya.

Mwili wake umekutwa nyumbani kwake mjini Kigali akiwa amefariki dunia. 

Haijajulikana kifo chake kimesababishwa na nini kwani hakuwa mgonjwa na wala hajapata ajali. Mwili wake umepelekwa monchwari ya kiislamu ya dispensari ya Rwampala kwa maombi ya familia yake kwani miili ya waislamu haihifadhiwi katika monchwari za kawaida kwa mujibu wa imani zao.

Taarifa za kifo cha Ndikumana zimethibitishwa na Muigizaji Irene Uwoya ambaye alikuwa mke wake wa ndoa na kufanikiwa kuzaa mtoto mmoja wa kiume.

Ndikumana na Uwoya walifunga ndoa Julai 2009 jijini Dar es salaam katika kanisa la Mt. Joseph, na walitengana baada ya  muda mfupi.

0 comments:

Post a Comment