Pages

Subscribe:

Sunday, December 20, 2015

BEN POL ATOA SABABU YA KUMWANDIKIA ALIKIBA TWEET ILIYOZUA UTATA

Ben Pol amesema tweet ya utata aliyomuandikia Alikiba, alikusudia kumtumia kwenye ujumbe wa siri wa mtandao wa Twitter (DM) lakini akakosea na kuiweka wazi!
Juzi kupitia mtandao huo, Ben Pol alimuuliza Alikiba swali, “Bro @OfficialAliKiba mi naona kama unakuwa overrated halafu inakugharimu...

au Haikugharimu?”

Ben Pol ameiambia Bongo5 kuwa wasanii wamekuwa wakiambiana ukweli kuhusu muziki na maisha yao ili kuwekana sawa.


“Ile tweet kwanza nilikuwa nataka iende DM,” alisema.
“Unajua sisi wasanii tunaongeaga tu, mtu anaweza akakwambia ‘mwanangu mbona hauna kiki.’ Kwahiyo mimi nilikuwa naipeleka ile tweet DM, lakini nikaipost kimakosa ikaenda public,” alifafanua.

“Mimi pale kitu kimoja kimenichanganya, watu wengine wamesema poa, wengine wanasema hapana, wengine wanatukana kwahiyo kwa kifupi hali imekuwa tafrani.”

“Sasa Ali alivyoona labda na yeye amelipokea vibaya baada ya kuona nimeweka public ndio maana akajibu namna ile. Kwa sababu hajanipigia akaniuliza mbona mwanangu umeandika hivi? Ila yeye aliona kama noma na iwe noma. Mimi haijanigharimu, labda kwa sababu watu wanaandika vibaya kwenye mitandao ya kijamii lakini hii ni kawaida lakini nachotaka watu wajue nilitaka tweet iende DM. Sijawahi kugombana naye, hatupo pamoja mara nyingi lakini tupo pamoja,” aliongeza.

Katika hatua nyingine Ben Pol amewataka mashabiki wake kuitazama video ya wimbo wake ‘Ningefanyaje’ aliyoiachia wikiendi hii.

0 comments:

Post a Comment