Pages

Subscribe:

Wednesday, November 1, 2017

VANESSA MDEE ATUA KWENYE IMAYA YA CASSPER NYOVEST


Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Vanessa Mdee amezidi kuonyesha uwezo wake kwa upande wa ‘video queen’ mara baada ya kuonekana katika video ya rapper Cassper Nyovest kutoka nchini Afrika Kusini.

Juzi, October 30, 2017 Cassper Nyovest aliachia ngoma yake mpya hiyo ‘Baby Girl’ ambayo Vanessa...
ndio kachukua nafasi hiyo ‘video queen’.
Hii si mara kwanza kwa Vanessa kufanya hivyo, utakumbuka January 2015 alitokea kwenye video ya Jux katika ngoma ‘Sisikii’, baada ya hapo waliweza kutoka ngoma ya pamoja inayokwenda kwa jina la Juu.
Hata hivyo kuna uwezekana mkubwa Cassper Nyovest akapita katika nyayo za Jux kwa kuja kuachia ngoma na Vanessa. Akizungumza na Dj Show ya Radio One Vanessa amesema kuna muendelezo wa kazi kati yake na rapper huyo.

“Ni project endelevu tumeanza kwanza na video yake ya ‘Baby Girl’ ambayo nimecheza, so next msubirie kidogo itakuja very soon” amesema Vanessa.

0 comments:

Post a Comment