Rapa, Mwimbaji, mwandishi,
na mtunzi wa kazi za muziki kutoka Marekani, Kisean Anderson ‘Sean
Kingston’ amefichua juu ya ujio wa kazi yake mpya itakayomshirikisha
Staa wa muziki kutoka Nigeria Davido na Staa wa muziki Mkanada, Tory
Lanez.Jumamosi ya tarehe 17, kupitia mtandao wa Twitter, Kingston aliweka ujumbe kuwa kazi iliyoko njiani kutoka kwake inakwenda kwa jina la ‘Kryptonite’ na Afrika imewakilishwa na Davido katika wimbo huo, huku...
isibainike kama Tory Lanez karap, kaimba au kafanya mchanganyiko kwakuwa anaweza kote kote.

Davido na Tory Lanez
“My new single Kryptonite ft @torylanez x @iam_davido it’s on the way Currently getting Mixed & Mastered !!!!” alitweet Sean Kingston.
Hata hivyo kwa Davido kolabo hii haitakuwa mara yake ya kwanza kufanya na Staa au Mastaa wa Kimataifa kwakuwa alishafanya kazi na Tinashe, Meek Mill na Rae Sremmurd na Young Thug kwenye ‘Pere’ iliyotolewa hivi karibuni.



Follow on Instagram
0 comments:
Post a Comment