Pages

Subscribe:

Tuesday, October 25, 2016

JOH MAKINI: SIPENDI BIFU NA MSANII YEYOTE YULE


 
Msanii wa miondoko ya Hip Hop nchini Joh Makini amesema katika vitu ambavyo hapendi kwenye kazi zake za kisanii ni kuwa na 'bifu' na msanii mwenzake katika tasnia ya sanaa nchini. 

Makini ameyasema hayo alipokuwa akijibu maswali ya wapenzi wa muziki wa Bongo Fleva waliokusanyika kushuhudia program maalumu ya Kamatia Kitaa. “Sipendi kuwa na bifu na msanii yeyote , mimi naamini katika muziki wangu na kuheshimu...
kila mmoja katika kazi yake” Amesema Makini

Aidha Makini ameongeza kuwa katika mambo ambayo humuumiza sana ni kuona kazi za wasanii zikiwa zimezagaa mtaani na kuuzwa bila wasanii kunufaika na chochote.
“Jambo hili inabidi serikali iingilie kati kwa sababu ugumu wa maisha mtaani umefanya vijana kuanza  kudurufu kazi zetu na kuziuza bila sisi kunufaika na chochote na jambo hili linatokana na jamii kutokuwa na elimu ya kutosha “ Amesema Joh Makini.

Pamoja na hayo Makini amewataka mashabiki kuendelea kuwaunga mkono kwani kundi la weusi limejipanga vyema katika kutoa burudani ya uhakika kwa mashabiki.

0 comments:

Post a Comment