Pages

Subscribe:

Wednesday, October 26, 2016

WCB YAMUWAHI SHAA KUMSAINI MSANII ZOCCU


13703165_1682324148755567_1354955220_n
Label ya Shaa, SK Musik, ilizidiwa ujanja na Wasafi Records ya Diamond na kumwahi kumsainisha msanii wa huyu wa kike. Jina lake ni Zoccu. Mwaka jana alishiriki kwenye shindano la Tecno Own The Stage lililofanyika nchini Nigeria.

Akizungumzia wasanii aliowapata kwaajili ya kuwasimamia kupitia label yake, Shaa alisema alimpata Zoccu lakini akachelewa na hatimaye kukuta mwana si wake.
“Nilimpata bwana binti mmoja anaitwa Zoccu lakini nikawa...
kidogo nimechelewa chelewa nikawa namuambia mwakani mara nashangaa napita Wasafi Records namkuta Zoccu kashachukuliwa,” Shaa aliiambia Millard Ayo. 

Shaa amesema sasa anao wasanii wawili, Myler na mwingine kutoka Tanga na mwakani ataanza kuwatambulisha rasmi.

0 comments:

Post a Comment