Pages

Subscribe:

Wednesday, October 26, 2016

HIKI NDICHO ALICHO KISEMA MENEJA WA MAN FONGO KUHUSU SINGELI


“TAMAA YA WADAU ITAUA SINGELI” ndicho alichokimaanisha. Ni wasanii kadhaa tayari wameshanukuliwa wakionyesha kutokuwa na imani endapo muziki unaohit kwa sasa Singeli utafika mbali.

G maker ambaye ni manager wa Man fongo na alikuwa maneger wa Sholo mwamba pia amesema muziki wa singeli ili udumu unahitaji umoja na dhamira ya kweli na siyo kinachoendelea sasa hivi. G maker amesema...
amepokea simu mara kibao kutoka kwa media moja wakitaka kumchukua Man fongo ili wammiliki jambo ambalo anaona wanatafta kumtumia tu kisha watamtelekeza.
 
Kupitia Planet bongo ya EA radio amesema Tangu alivyowatoa Man fongo na Sholo mwamba kumekuwa na Vitisho kutoka kwa baadhi ya media na mvutano mkubwa wakiwataka wasanii hao jambo ambalo lilimshangaza na kujiuliza walikuwa wapi siku zote.

Mbali na hilo amesema singeli inahitaji umoja na wasanii wengi wa singeli hawajaenda shule sana kwa hivyo inakuwa rahisi kurubuniwa. “Kila mtu akitaka kuwatumia hawa watoto kupiga hela, utakufa kweli”.alisema Gmaker akitoa mfano wa style kama TAKEU ya Mr Nice na MCHIRUKU ambazo zimepotea.

0 comments:

Post a Comment