Pages

Subscribe:

Friday, October 28, 2016

KAULI YA MADEE JUU YA KASSIM MGANGA HUENDA AKARUDI TIP TOP

kassimmganga-20161028-0001
Msanii na gwiji wa tungo za mahaba kassim mganga uenda akasainiwa na Tiptop connection kwa kuwa ameshafanya mazungumzo ya awali na Madee ivyo anasubiri mazungumzo ya mwisho na manager wa kikosi hicho Babutale.

Madee akiongea katika kipindi cha ‘street joint’ ya Dizzim, amefunguka kuwa kassim alimfuata wakazungumza kuhusu yeye kujiunga na team hiyo, lakini hakuweza kumpa majibu yamoja kwa moja. Madee anasema bado ajalifikisha hilo kwa...
uongozi wa juu, kwa hiyo pindi litakapokuwa tayari atarudi tena kutueleza kama tayari jamaa kaisha jiunga na timu, ila kwa sasa hawezi liongelea sana.

Kassim mganga ameonekana pichani siku chache akiwa morogoro katika harusi ya Tundaman mkali mwingine wa Tip top.
Madee amedai alifurahishwa kumkuta kassim kule, tena kamkuta kama msemaji anae wawakilisha.

0 comments:

Post a Comment