Pages

Subscribe:

Thursday, October 27, 2016

JOKATE ATAJA SABABU ILIYOFANYA TZ KUKOSA TUZO ZA MTV


jokate-2
Super business woman, Jokate Mwegelo aka Kidoti amefunguka sababu anayodhani ilifanya wasanii wa Tanzania washindwe kushinda tuzo za MTV MAMA zilizofanyika Jumamosi iliyopita nchini Afrika Kusini.

Mwanamitindo huyo alikuwa akijibu swali la mmoja wa mashabiki wake kwenye mtandao wa Twitter, lililokuwa likiuliza “Je ni kweli...
U-team ulitucost tuzo za MAMA’s mwaka huu?”
Jokate alijibu swali hilo kwa kuandika, “Sio Kweli, hatukuwa na nyimbo kali iliyotamba maeneo mengi ya Afrika.”
jokate
Kidoti aliongeza kuwa u-team bado unahitajika kwaajili ya kuleta ushindani imara. Mwanamitindo huyo anadaiwa alikuwa ni miongoni mwa watu waliohudhuria kwenye utoaji wa tuzo hizo kwenye ukumbi wa Ticketpro Dome nchini humo.

0 comments:

Post a Comment