Pages

Subscribe:

Wednesday, October 26, 2016

NYUMBA YA DIAMOND YAMTOA POVU H-BABA AFUNGUKA HAYA


Kama wewe ni mtumiaji wa mitandao ya kijamii najua ilikufikia hii ya Team za mastaa wawili wa muziki hapa nchini Team Diamond & Team Kiba kutishiana nyumba za mastaa wao hapo jana.




Ni baada ya msanii Diamond Platnumz kuposti mjengo wake katika ukurasa wake wa Instagram na kuandika maneno flani hivi ambayo yametafsiriwa kama vijembe, ndipo msanii H-Baba alipoibuka na kuachia...
comments kuihusu nyumba hiyo na akidai kuwa kama Diamond anataka kuwaaminisha watu kuwa nyumba hiyo ni yakwake basi aposti  na hati ya nyumba ili watu waweze kuamini.
Instagram photo by Udakutz.Com_BMA1gy4DEZQ - JPG
Ndipo Soudy Brown alipoona sio kesi na kuamua kumvutia waya mkongwe huyo. Na alichokisema H-Baba unaweza kukisikiliza kwa kutazama hiyo video hapo chini.
Soudy Brown hakuishia kwa H-Baba tu, bali aliamua kumvutia waya na Alikiba ili kutaka kujua ukweli kuhusu ile nyumba ambayo ilipostiwa na Team Kiba ni yakwake kweli au la! Alikiba ameikana vikali nyumba hiyo na kudai kuwa hata kama ingekuwa ni yakwake asingeweza kuianika mtandao ni kwa sababu yeye sio mtu wa aina hiyo.

Alikiba alimaliza kwa kusema kuwa yeye anaishi kwenye nyumba ya kupanga.
Punguza presha, ubuyu wote nimekukusanyia hapa chini kwenye video hii, play uweze kuumung’unya taratibu bila hofu kisha ukawahadithie na wenzio.

Watch Here 

0 comments:

Post a Comment