Pages

Subscribe:

Monday, January 23, 2017

NAY WA MITEGO: SIKUNGA NA MAMA MIAKA MITANO

Rapa Nay wa Mitego ambaye anafanya vyema na wimbo wake 'Sijiwezi' amefunguka na kusema kuwa ni kweli alikuwa amezinguana na mama yake mzazi na walikaa miaka mitano bila kupiga stori yoyote ile. 
 
Nay wa Mitego alisema haya kupitia kipindi cha Planet bongo na kusema kwa sasa wameshamaliza tofauti zao na anaishi na mama yake mzazi ingawa anakiri kuwa ni kweli ameishi... zaidi ya miaka mitano bila kuongea na mama yake mzazi.
 
"Mimi na mama mzazi tuko poa sana na nina kaa naye this time, ni kweli kabisa tumekaa miaka mitano bila kuzungumza jambo lolote lile ila ni mazingira ya maisha ya mtaa niliyokuwa naishi lakini mpka muda huu tunaongea mimi naishi na mama yangu nyumbani kwangu, hivyo niko naye nyumbani" alisema Nay wa Mitego

Mbali na hilo Nay wa Mitego anasema yeye haamini katika dini kwani anaona dini nyingi saizi zimekuwa biashara, hivyo yeye anamini Mungu na anajua Mungu yuko kila sehemu si lazima iwe kanisani.

0 comments:

Post a Comment