Pages

Subscribe:

Friday, January 6, 2017

DARASSA AMTAJA PRODYUZA ALIYE WAHI KUMTOSA

Rapa Darassa amefunguka na kuweka wazi jambo ambalo katika maisha yake ya muziki lilimkwaza sana na hataweza kulisahau ni baada ya mmoja wa Producer wake kutoka AM Record Manecky kumkatalia kufanya kazi ambayo ndiyo iliweza kufungua zaidi milango.

Darassa anakiri kuwa AM Record kwake ndiyo ilikuwa kama nyumbani kutokana na kazi alizokuwa akifanya lakini anadai aliweza kufanya kazi kwa Mr T Touch na siku hiyo studio ya...
T Touch kulikuwa na matatizo hivyo ilibidi ampigie simu Manecky na kumuomba waende studio ili waweze kupata sauti ya Mr Blue lakini mwisho wa siku Manecky alimkatalia.

“Sijawahi kusema hilo jambo sehemu yoyote ile ila nakumbuka siku hiyo nilikuwa nimefanya kazi kwa Mr T Touch ila studio kulitokea matatizo kipindi hicho mimi naunga unga hivyo nilimpigia simu Manecky nikiamini AM Record ni nyumbani kweli aliniambia niende nikaenda na Mr T Touch pamoja na Mr Blue lengo lilikuwa nipate tu sauti ya Mr Blue kisha ile kazi akamalizie Mr T Touch lakini huwezi amini Manecky alinikatalia”. Alisema Darassa

Mbali na hilo Darassa anasema wimbo ambao ulimpeleka kwa Manecky ndiyo wimbo ambao uliweza kufungua milango zaidi katika muziki wake

0 comments:

Post a Comment