Pages

Subscribe:

Sunday, January 22, 2017

HII NDIYO KAULI YA FID Q BAADA YA KUIONA POST YA MH PAUL MAKONDA

Kwenye ile orodha ya mashabiki wa damu wa Mwanahiphop Fid Q inabidi umuongeze na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda ambaye January 20 alitumia time yake kupost kipande cha video ya Fid Q na kuandika: ’Hakika umetubeba hakuna bingwa na mbabe ktk anga hizi kama wewe, huna mbwembwe na ujumbe unafika’ #Mzikimgum

Baada ya Fid Q kuiona hiyo post amemshukuru Paul Makonda kwa kuandika ‘Shukrani sana Mheshimiwa mwenye DAR yake @paulmakonda – kiukweli...
tunajivunia kuwa na kiongozi kijana na mchapakazi kama wewe’

‘Kinachotukosha zaidi ni vile unavyoutumia muda wako wa mapumziko vyema kwa kufuatilia na kusapoti kazi za sanaa za vijana wa taifa letu kama mimi’ – Fid Q

 
Ubarikiwe zaidi bro.. Na kama utapata muda usisahau kuclick kwenye ile LINK iliyopo kwenye BIO yangu.. kuna NGUMU nyingine mpya inaitwa ‘ KEMOSABE ‘ nimeiweka jana.. yote na yote mkuu.. Asante sana kwa #loveyahelayote

0 comments:

Post a Comment