Pages

Subscribe:

Thursday, January 5, 2017

KALAPINA ADAI CHID BENZ ANAHARIBIWA NA MAMA YAKE


kalapina-20161007-0001
Rapa Kalapina ambaye ni mwanaharakati wa kuwasaidia watu ambao wameingia kwenye matumzi ya dawa za kulevya amefunguka na kumtaja mama yake mzazi Chid Benz kama mtu anaye muendekeza Chid na kumfanya asitoke kwenye matumizi ya dawa za kulevya.

Kalapina adai mama huyo anampenda sana mtoto wake kiasi cha mtoto kujua na kuona kwamba hata akifanya jambo fulani yupo mama yake ambaye...
atasimama na yeye.

Kalapina alisema wazazi wengi wamekuwa chanzo cha watoto wao kuingia kwenye matumzi ya dawa za kulevya na kuingia hata kwenye mahusiano ya jinsi moja sababu ya wazazi wamekuwa wakiwadekeza sana watoto au kuwapa uhuru mkubwa na kuruhusu maisha ya uzungu kutawala.

“Kiukweli mama yake mzazi Chid Benz anampenda sana mwanaye na hali hiyo inampelekea mdogo wangu yule kuona hata nikizingua mama atanitafuta tu, au kuona mama atasimama na yeye tu sababu mama yake anampenda sana, lakini siyo Chid Benz tu wazazi wengi wanawalea watoto kwa kuwadekeza sana”. 

Aliongeza, “wazazi hawana muda na watoto na hili linachangia vijana kuingia kwenye madawa ya kulevya hata kwenye ushoga pia, lakini sisi wazazi wetu zamani ulikuwa ukizingua unapigwa sana hivyo lazima utanyooka tu” alisema Kalapina kwenye Planet Bongo ya EA Radio.

0 comments:

Post a Comment