Pages

Subscribe:

Tuesday, December 20, 2016

MASHABIKI WAMSHAMBULIA DIAMOND KISA AJALI YA DARASSA


Ikiwa bado ngoma ya muziki toka kwa Darasa ikitrend, mengi yanazidi kuibuka na story kibao zinaandikwa kuhusu Darasa na muziki wake. 

Juzi kati hapa, mshikaji wetu Darasa alipata ajali alipokua anaelekea kwenye show Kakola, yeye pamoja na director wake huku wakiambatana na producer wake walinusurika na kutoka salama kabisa, kupitia ukurasa wake wa instagram...
, Darasa aliandika haya:

God apewe sifa

kiwanda cha uzalishaji #MUZIKI kipo salama kabisaaaaa ndani ya KAKOLA leo mtaenjoy #MUZIKI

Wasanii,wadau pamoja na mashabiki walitumia muda wao kumpa pole kutokana na ajali hiyo, wengi waliandika kwenye kurasa zao za mitandao kama facebook na instagram.

C.E.O wa WCB wasafi Diamond Platnumz kupia ukurasa wake wa instagram, aliandika kumpa pole Darasa kutokana na ajali hiyo ndipo maneno mengi yakaibuka kutokana na post hiyo,comments za aina tofauti tofauti ziliandikwa huku nyingi zikionekana kumshambulia Diamond kwa kile kinachodaiwa kua hajawahi kumsupport Darasa kwa kupost cover ya ngoma inayotembea kwa sasa ya Muziki

Mashabiki wanadai Diamond amesubiri ajali tu wakati ngoma ni kubwa na hajawahi kumpongeza Darasa, imekua kama debate kwasababu kuna wengine wanadai hata Darasa hajawahi kumpost Diamond, wanaona sio fresh kumtuhumu Diamond pekee wakati wawili hao hawana mazoea ya kutupiana post kwa page zao.

0 comments:

Post a Comment