Pages

Subscribe:

Monday, December 19, 2016

HII NDIYO TAARIFA YA POLISI KUHUSU AJALI ALIYOPATA DARASSA



Abbah, Mr Vs, Darassa na Hanscana wote wame nusurika kwenye ajali hiyo
December 18 Rapa Darassa aliripotiwa kupata ajali akiwa safarini kutokea Kahama ambako alikua na show wikiendi iliyopita, Jeshi la Polisi Tanzania kupitia mkoa wa Shinyanga wametoa taarifa ya ajali hiyo ikiwemo chanzo chake cha ajali.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI (M) SHINYANGA KWA VYOMBO VYA HABARI. 18/12/2016
AJALI YA GARI KUACHA NJIA , KUPINDUKA, KUSABABISHA MAJERUHI NA UHARIBIFU WA GARI. TAREHE 18/12/016 SAA 15:00, HUKO KATIKA...
KIJIJI CHA NTOBO, KATA YA NTOBO, TARAFA YA MSALALA , (W) YA KAHAMA MKOA WA SHINYANGA, GARI REG NO T 503 DGQ TOYOTA DARK BLUE HARRIER MALI YA SHARIF S/O THABIT RAMADHAN @DARASSA BOXDSM, MNYAMWEZI ,MIAKA 28 , IKIENDESHWA NA YEYE MWENYEWE ILIACHA NJIA, KUPINDUKA NA KUSABABISHA MAJERAHA KWA SWITBERT S/O CHARLES ,MSUKUMA ,MIAKA 24 , PRODUCER WA MUZIKI, MKAZI WA DSM AMBAYE AMEPATA MICHUBUKO MIKONO YOTE MIWILI, PIA KUSABABISHA UHARIBIFU MKUBWA WA GARI HILO. MAJERUHI AMETIBIWA KITUO CHA AFYA CHA MGODI WA DHAHABU BULYANHULU NA HALI YAKE INAENDELEA VIZURI .CHANZO CHA AJALI HIYO NI MWENDO KASI WA DEREVA WA GARI HILO. HATUA ZINGINE ZA KISHERIA ZITAFUATA.. RPC SHINYANGA.

Kwamujibu wa Bongo5 Jumatatu hii imeripoti kuwa,  Hanscana amedai hajui chanzo cha ajali hiyo huku akidai hata yeye anashangaa kwani walikuwa kwenye mwendo wa kawaida sana.

“Dereva alikuwa Darassa wakati tunapata ajali na kusema kweli tulikuwa kwenye mwendo wa kawaida sana, ghafla tukashangaa kuona gari ina serereka na kupinduka mara nne. Kwa hiyo ni ajali kama ajali nyingine sema sisi tunashangaa mazingira ya ajali lakini yote ya yote tunamshuru Mungu kwa sababu wote ni wazima,” alisema Hanscana.
Aliongeza, “Kwa sasa tunaangalia namna gani tunaweza kurudi Dar es salaam kwa sababu huku tuliko ni mbali sana na tulikuja kwa ajili ya show,”.
Hizi ni baadhi ya picha kutoka kwenye Ajali hiyo siku ya Jana


0 comments:

Post a Comment