Pages

Subscribe:

Tuesday, November 29, 2016

ALI CHOKI: NITAPUMZIKA TU LAKINI SITAACHA MUZIKI

Jumamosi hii mwanamuziki wa dansi nchini tanzania Ali Choki ametimiza miaka 30 ya muziki wake na amewashukuru wasanii ambao alishirikiana nao katika kipindi chote hicho cha muziki wake. 

Akiongea ndani ya eNewz Ali Choki amesema anashukuru kwa 'kampani' aliyoipata kutoka kwa wanamuziki wenzake kama Zahir Zoro, Komando Hamza Kalala na wengine lakini pia aliamua kupiga nyimbo za...
Extra Bongo ili kuonesha maana ya halisi ya miaka  30 ya Choki.

Hata hivyo Choki amesema huenda akapumzika baada ya miaka 20 ijayo mbele japo hawezi kusema rasmi kwamba ataacha muziki kwa kuwa siyo rahisi kustaafu muziki kwani muziki  ni kipaji chake labda akifikisha miaka 50 ya muziki.

0 comments:

Post a Comment