Pages

Subscribe:

Tuesday, November 29, 2016

CHRISTIAN BELLA: WIMBO WANGU NA KOFFI TULIUTOA BILA PLAN


14499068_1749552105295206_1176540174012645376_n
Christian Bella amefunguka sababu ya wimbo wake ‘Acha Kabisa’ aliomshirikisha Koffi Olomide kutofanya vizuri. Muimbaji huyo amekiambia kipindi cha Clouds E cha Clouds TV kuwa waliuuachia wimbo huo bila plan wala kuutangaza ndio maana haukufanya vizuri.

“Ngoma tulivyorekodi hatukuifanyia promosheni, siku zote muziki hauwezi kufa. Ninaweza kusema kuwa tuliitoa bila plan kwa sababu Koffi alikuwa anakuja ndio tukaitoa, lakini ngoma ni nzuri tukiifanyia kazi na tukiiboosti kwa...
video nzuri itapata nafasi yake. Mimi naamini ni ngoma nzuri lakini Koffi kumuelewa ilikuwa ngumu kidogo kwa sababu aliimba full kikongo,” amesema.

Hata hivyo Bella ameongeza kuwa atafanya kazi nyingine na mkongwe huyo wa muziki wa dansi.

0 comments:

Post a Comment