Pages

Subscribe:

Thursday, November 24, 2016

DITTO AFUNGUKA SABABU YA YEYE KUWA KIMYA KIMUZIKI KWA MUDA MREFU

Ukiizungumzia Tanzania House of Talent (THT) ni lazima uwataje watu muhimu ambao wamewekeza nguu zao na kuibua vipaji vingi sana vinavyo fanya vizuri kwenye tasnia ya bongo.
 
Lameck Ditto ni miongoni mwa wasanii waliofanya kazi kubwa ya kuwaanda wasanii wengi kwenye chuo hicho cha vipaji hapa nchini.Ditto pia ni msanii ambae aliwahi kutamba na ngoma zake kadhaa zilizoipa heshima kazi yake na...

wasanii walinyuma yake.

Bongoswaggz inakusongezea sababu zilizomfanya kuwa kimpya kwa muda mrefu kabla ya kuachia 'Moyo'

"Niliamua kutoachia ngoma ili tu nipumzike na nijaribu kuandika kazi nyingi. na pia niwaandikie watu wengine ili nikija kuanza kuachia ngoma niachie nyimbo kwa mfululizo.na pia nilikuwa kimya kwasabbu nilikuwa nawaandikia wasanii wengi,nyimbo kama Maumivu ya Kadjanito,Malkia wa nguvu ya Linah na nyimbo nyingi za mashirika." alisema Ditto.

Je? unawajua wasanii waliotokea katika jumba la sanaa tanzania (THT), smashkilimanjaro inakupa list fupi ya wasanii hao ni Barnaba, Amini, Ditto,Maua Sama, Ruby, Msami, Linah, Alice na wengine wengi wote ni vizazi vyema vya THT.

0 comments:

Post a Comment