Pages

Subscribe:

Monday, November 28, 2016

Lyrics: Mwana FA ft Vanessa Mdee_Dume Suruali (Mashairi)

mwana-fa
Mwana FA
Hudat hudat hii ni salam na ufahamu
Kama unauza mapenzi siyo kwa binamu
Huna haja ya kusubiri hii ni hukumu
Hakuna kitu utapata utangoja kama askari wa zamu
Dume suruali dume kaptula
Shauri zako ilimradi sipati hasara
Usione utani me sihongi hata kwa ishara
Utaniambia nini mpaka unigeuze fala
Kwanza nasikia hongo zinaleta mkosi...

Sentano yangu hugusi hata ukiongea kidosi
Yabaki mapenzi tusileteane ujambazi
Hata upige sarakasi utachonga viazi.
BAHILI KAMA NINI!!!!!!!!! Ndiyo mnavyosema
Na ukiniomba kesho hunisikii tena
Kwani unauza nini dada!
Hunitakii mema.

Kiitikio

We dume suruali kaa mbali nami
Kama dume suruali kaa mbali nami
Huendani na mimi
I want Gucci, Fendi, spend it on the girl like me
My name is Vee Money, money spend on the girl like me

MWANA FA
Nihonge nanunua nini kwa nini yaani!
Kuna kipi nisichokijua ina TV ndani?
Usiulize n’takupa nini dada piga moyo konde
Viuno vingi kama mwali wa kimakonde
Usipende hela kama mfuko
Au fanya unavyofanya upate zako
Vishawishi vingi binti sema na moyo wako
Na ujifunze pesa zinauza utu wako
Tajiri mtata kama Salah
Zipo ila sitoi me ni balaa
Unapenda hela zangu nami nazipenda pia
Kila mtu abaki na zake bye baby tutaongea
MWANAUME WA HIVYO WA NINI SASA!!!!! Ndiyo mnavyosema
Na ukiniomba kesho hunisikii tena
Kwani unauza nini dada
Hunitakii mema

Vanessa
Aje aje ajeeee me mtoto fulani ghali
Nihonge gari Ma sweet sweet baby
Wanna see you today unipeleke party
Aje aje ajeee njoo nikupe TBT

MWANA FA
Siyo kwa enzi ya Magufuli
Zali ilikuwa long siku hizi hakuna la mentali
Nikikuhonga na ukiniacha nitakujia usingizini
Naepusha shari matatizo yote ya nini
Hakuna kipya chini ya jua
Hata nisiyoyafanya nishayasikia
Ningekuwa mhongaji ningeshafulia wangu
Mademu wangu wa zamani wote wangekuwa maadui zangu
MWANAUME HOVYO WEWE!!!!! Ndiyo mnavyosema
Na ukiniomba kesho hunisikii tena
Kwani unauza nini dada
Hunitakii mema

Vanessa
Baki na hamu zako

Kiitikio
We dume suruali kaa mbali nami
Kama dume suruali kaa mbali nami
Huendani na mimi
I want Gucci, Fendi, spend it on the girl like me
My name is Vee Money, money spend on the girl like me

VANESSA
Baba bure huyuu!!!

Mwana FA
Hata pantoni lina staff
Vanessa
Unamwambia nani sasa! Unamwaaambia nani sasa!

0 comments:

Post a Comment