Pages

Subscribe:

Wednesday, April 5, 2017

EDU BOY: SIJAMUIMBA MADEE KWA NIA MBAYA

Msanii wa Hip Hop anayewakilisha Mwanza, Edu Boy amejitetea kupitia Planet Bongo ya EATV kuhusu mstari aliomtaja msanii wa 'Tip Top Connection' Madee kwamba hakumtaja kwa nia mbaya bali alimuweka ili kuonesha jinsi gani msanii huyo alimfungua macho 

Edu Boy amesema kwamba lengo la kumtaja madee kwenye wimbo wake ni kwa sababu kuna kipindi alimuomba amsaidie kumtoa kimuziki lakini alimshauri aendelee na....
kujifua hadi muda wake wa kutoka utakapofika.

"Madee yupo real sana. niliwahi kumpigia simu wakati Dogo Janja kazingua nikamwambia mimi ni mkali nisaidie maana nina uwezo kuliko Janja akaniambia hebu chana nilipomchania akaniuliza uko wapi nikamjibu nipo Mbagala akaniambia basi kama unapenda kuimba endelea kujifunza zaidi au endelea kutungua nazi, kuanzia hapo nilikaza baada ya jibu lile" AlisemaEdu Boy.

Aidha msanii huyo ameongeza kwamba wasanii wote ambao amewataja kwenye ngoma yake aliyomshirikisha Billnass 'Naiee' hazikuwa 'diss' za uongo bali aliamua kutoa ya moyoni kupitia wimbo huo kwani watu wote aliowataja aliwahi kuwaomba msaada wakakaza na wengine kumtolea maneno machafu.

0 comments:

Post a Comment