Pages

Subscribe:

Wednesday, April 5, 2017

STORY: SI KITU BILA PENZI LAKO-12

Image result for WALK AWAY
Alijulikana kwa jina la Gabriel Smith, mchungaji ambaye alikuwa akitokea katika nchi ya Marekani ndani ya jiji la New York. Mchunngaji Smith alikuwa na kanisa kubwa kuliko kanisa lolote katika jiji la New York. Kila siku kazi yake ilikuwa ni kuhubiri Injili katika sehemu mbalimbali duniani.

Hakuwa akitulia kanisani kwake, mara kwa mara alikuwa akisafiri kuelekea katika nchi mbalimbali kuhubiri Injili. Katika kila nchi ambayo alikuwa akienda, wagonjwa...

waliponywa na hata wenye shida mbalimbali waliombewa.

Jina lake likawa kubwa miongoni mwa wachungaji wakubwa duniani kama Benni Hinni, Td Jakes na wahubiri wengine. Miujiza mbalimbali ambayo ilikuwa ikifanyika katika mikutano mbalimbali aliyokuwa akihubiri ndio ambayo ilimfanya kujulikana zaidi.


Katika maisha yake alibahatika kupata watoto watatu tu, wa kwanza alikuwa James ambaye alikuwa mwanasheria wa kujitegemea na ambaye alianzisha kampuni yake mwenyewe nchini Marekani. Wa pili alikuwa Mickey ambaye alikuwa akicheza mchezo wa kikapu katika timu ya Heart nchini Marekani na wa mwisho alikuwa Lydia ambaye bado alikuwa akiishi nae.
Katika maisha yake yote, mchungaji Smith alikuwa na mke mmoja ambaye alipata nae watoto hao wote, mwanamke huyu aliitwa Elizabeth.


Elizabeth alionekana kuwa kila kitu katika maisha yake, alimpenda mwanamke huyu kuliko mwanamke yeyote katika dunia hii kwani yeye ndiye ambaye alikuwa akimpa furaha kila siku na kujiona mtu muhimu katika dunia hii.


Kila alipokuwa akisafiri kuelekea katika mikutano mbalimbali ya kimataifa, mchungaji Smith alikuwa akienda sambamba na mkewe, Elizabeth. Ingawa walikuwa na umri mkubwa lakini mapenzi yao bado yalikuwa yakionekana kuwa makubwa tofauti na wale watu ambao walikuwa wameanza uhusiano katika siku chache zilizopita.


Ukarabati wa eneo la kaburi la Nyerere ulikuwa umetangazwa katika vituo mbalimbali duniani. Kaburi lile lilikuwa limefanyiwa ukarabati na kuwa sehemu mojawapo ya kufanyia utalii kwa ajili ya kumbukumbu ya kumuenzi Baba wa Taifa.
Mchungaji Smith hakutaka kubaki nchini Marekani, nae akatamani kwenda huko kuangalia ukarabati huo ambao ulikuwa umefanyika.


Kwa kipindi kirefu sana alikuwa akimfahamu vilivyo marehemu Nyerere. Alipokuwa shuleni hasa chuoni miaka ishirini iliyopita, alikuwa akisoma mambo mengi kuhusu mtu huyo. Aliimpenda sana hasa na moyo mkubwa wa kujitoa aliokuwa nao katika kuutafuta uhuru wa nchi ya Tanganyika pamoja na nchi nyingine za jirani.


Mchungaji Smith akajiona kuwa na umuhimu wa kwenda Tanzania kwa ajili ya kuona kile ambacho kilikuwa kimetangazwa na ambacho kilitakiwa kufanyika katika siku ya tarehe 14 mwezi wa 10 mwaka 2000.


Kwa kuwa binti yake, Lydia alikuwa nyumbani, akaamua kusafiri nae na kuelekea katika nae nchini Tanzania pamoja na mkewe. Akaanza kupiga simu kwa rafiki yake ambaye walikuwa wamezoeana kwa kipindi kirefu, mtanzania Gibson ambaye mara kwa mara alikuwa akimpokea kila alipokuwa akielekea nchini Tanzania.


Mara baada ya kufika nchini Tanzania kisiri pasipo watu wa makanisa kujua kama yuko nchini Tanzania, safari ya kuelekea mkoani Musoma katika kijiji cha Butiama kuanza. Hawakutaka kupanda ndege, walitaka kusafiri kwa kutumia gari kwani walitaka kupitia katika mbuga kubwa ya wanyama ambapo hapo wangechukua vyumba na kisha kuendelea na safari yao na baadae kurudi katika hoteli hiyo.
*****
Mchungaji Smith, mkewe, Lydia na walinzi walikuwa wakiendelea kupiga hatua kulekea kule ambapo Lydia alikuwa akidai kwamba alimwona mzimu. Walitembea kwa hatua za haraka haraka huku mchungaji Smith akiwa na hamu ya kuuona mzimu wenyewe ambao Lydia alikuwa ameuona.


Walifika katika gari lile, boneti la gari lilikuwa wazi. Lydia hakusogea zaidi ya kunyooshea gari lile kidole. Gibson na mkewe, Beatrice wakafika mahali hapo na kutaka kujua ni kitu gani kilichokuwa kinaendelea. Mchungaji Smith akaanza kupiga hatua kuelekea kule kulipokuwa na gari lile, alipofika akachukua tochi yake na kumulika garini.


Patrick alikuwa akionekana amelala garini huku akionekana kutokujitambua kabisa. Mchungaji Smith akasogea karibu zaidi na zaidi na kuupeleka mkono wake ndani ya boneti lile la gari na kumgusa Patrick huku akijaribu kumtingisha lakini Patrick hakushtuka.


Mchungaji Smith akalifungua vizuri boneti lile la gari na kisha kujaribu kumtoa Patrick. Gibson akaja na kusaidiana nae. Mwili mzima wa Patrick ulikuwa umejaa mavumbi, alionekana kutisha kupita kawaida. Walinzi waliokuwa mahali pale wakambeba Patrick mpaka katika sakafu na kuanza kupepea.


Patrick alikuwa kimya, alionekana kupoteza fahamu kutokana na vumbi alilokuwa amelipata pamoja na udogo wa hewa ambao alikuwa akiupata. Wakaanza kumpa huduma ya kwanza huku mchungaji Smith akiomba Mungu Patrick afumbue macho yake na kuangalia tena.


Kama Patrick angekufa kwa wakati huo, tayari alijiona kuwa katika wakati mgumu kwa kuwa kusingekuwa na uthibitisho wowote kama Patrick alikuwa ameingia mwenyewe katika boneti lile. Watanzania wote wangeamini mchungaji Smith ndiye ambaye alkuwa amemuweka Patrick katika boneti lile.
“Hivi kuna hospitali hapa?” Gibson aliwauliza walinzi.
“Hospitali! Hospitali mbugani! Wala hakuna” Mlinzi mmoja alijibu.
“Kwa hiyo hakuna?”
“Ndio. Labda mpite mbuga kwa mbuga mpaka Arusha” Mlinzi aliwaambia.
Baada ya kumpa Patrick huduma ya kwanza, moja kwa moja safari ya kuelekea jijini Arusha ikaanza. Safari ilikuwa ni mbuga kwa mbuga lakini gari lilikuwa likiendeshwa kwa mwendo wa kasi pasipo kujali mashimo ambayo yalikuwa katika barabara hiyo ya vumbi.


Bado Patrick alikuwa hajafungua macho, aliendelea kulala katika usingizi wa kifo. Vumbi jingi lilikuwa limeingia katika mapafu yake, hewa ndogo ambayo alikuwa akiipata kule katika boneti la gari ndilo ambayo ilikuwa imempa hali mbaya zaidi.


Mpaka wanafika Arusha, tayari ilikuwa imetimia saa kumi alfajiri. Moja kwa moja wakaanza kuelekea mjini mpaka katika hospitali ya Kilutheri ya Selian ambako Patrick anapelekwa hadi katika chumba cha peke yake na kupewa huduma.
Ndani ya masaa mawili, Patrick anarudiwa na fahamu. Kila mmoja akaonekana kufurahia, hawakuamini kama Patrick angeweza kurudiwa na fahau kwa haraka namna ile.
“Tunamshukuru Mungu” Mchungaji Smith alisema.


Wote wakashikana mikono na kuanza kumshukuru Mungu. Sala ya shukrani iliendelea mahali hapo kwa dakika kadhaa. Muda wote huo Patrick hakuwa akielewa ni kitu gani kilikuwa kinaendelea mahali hapo, akabaki akishangaa tu.


Baada ya kuulizwa ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea, Patrick anaanza kueleza kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika maisha yake. Kila mtu hakuamini kile ambacho alikuwa amekisikia kutoka kwa Patrick. Bi Rachel hakuweza kuvumilia, akabaki akilia tu.
“Inasikitisha” Mchungaji Smith aliwaambia.
“Lakini ni kijana mdogo sana”
“Ndio. Ni lazima tumsaidie. Ni lazima uondoke nae Gibson. Ishi pamoja nae ili asiwe katika hali hii ya mawazo kwani kichwa chake naamini hakiko sawa. Jaribu kumfariji kila siku. Mimi na mke wangu tunaahidi kumsaidia katika kipindi ambacho atakuwa kwako” Mchungaji Smith aliwaambia.
“Sawa mchungaj. Hakuna wasiwasi” Gibson alisema.


Mchungaji Smith hakuendelea kukaa mahali hapo. Safari ya kuelekea nchini Marekani ikaanza. Walichukua ndege kutoka Arusha ambayo iliwapeleka mpaka Dar es Salaam ambako wakachukua ndege ya shirika la Emirates na kuelekea Marekani ambako kulikuwa na mkutano mkubwa katika jiji la Los Angels.


Ndani ya ndege bado walikuwa wakikumbuka historia ya maisha ya Patrick ambayo aliwaambia, kila mmoja akaonekana kuguswa na historia ya maisha ya Patrick. Wakaiahidi mioyo yao kumsaidia Patrick katika hali yoyote watakayokuwa nayo.
“Ni lazima tumsaidie. Ni lazima tutume dola elfu moja kila mwezi kwa ajili yake” Mchungaji Smith alimwambia mkewe.
“Kweli kabisa. Ni lazima tufanye hivyo. Najua Mungu ana makusudi na maisha yake” Bi Rachel alisema.


Kiasi ambacho kilikuwa kimetajwa kwa ajili ya kummsaidia Patrick kilikuwa kiasi kikubwa cha fedha hasa kama kingewekwa katika thamani ya fedha ya kitanzania.
Kiasi cha zaidi ya shilingi milioni mbili ndicho ambacho kilikuwa kimepangwa kwa ajili ya kumsaidia Patrick ambaye alitakiwa kuishi nyumbani kwa Gibson jijini Dar es Salaam. Mchungaji Smith na mkewe, Rachel walikuwa wakiendelea na safari yao huku mioyo yao ikijua kwamba huku Tanzania kulikuwa na mtu ambaye waliahidi kwa mioyo yao yote kumsaidia.


******

Hidifonce alitulia kitandani, hakuonekana kufurahishwa na kile ambacho alikuwa amemfanyia Maria. Alijua fika kuwa moyo wa binti huyo ulikuwa katika mapenzi mazito juu yake. Akaanza kuyajutia maneno ambayo alikuwa ameongea mbele ya Maria, hata yeye hakuonekana kufurahishwa nayo.

Hidifonce akainuka na kuanza kutembea tembea chumbani kwake huku akionekana kuwa na mawazo juu ya Maria. Muda wote alikuwa akipigapiga mikono yake huku macho yake yakiangalia darini. Alikuwa katika hali ile kwa muda fulani, akarudi tena kitandani.
“Haiwezekani, ni lazima nimuite” Hidifonce alisema na kisha kutoka nje ya chumba kile.


Moja kwa moja akamtafuta Shania na kisha kumtuma kwenda kumuita Maria. Shania akaondoka mahali pale na kuelekea nyumbani kwa mchungaji Christopher ambako baada ya dakika kumi, akarudi pamoja na Maria ambaye alikuwa katika hali iliyojaa furaha.


Moja kwa moja akaingia katika chumba cha Hidifonce na kutulia. Macho yake yalikuwa yakiangalia chini kama kawaida yake, alikuwa akijisikia aibu kiasi ambacho hakuweza kukutanisha macho na Hidifonce. Hidifonce alikuwa ametulia huku macho yake yakiendelea kumwangalia Maria, akaanza kujisogeza karibu nae.


Mkono wake akaupeleka shavuni mwa Maria na kuanza kulishika shika shavu lake. Maria akaanza kusisimka, mguso wa Hidifonce ukaonekana kuanza kumletea hali ya tofauti mwilini mwake. Hidifonce akaonekana kugundua hali ile, akazidi kusogea karibu zaidi. Akamgeuzia Maria upande wake na kuanza kumwangalia vizuri usoni.
Hidifonce akaanza kuusogeza uso wake karibu na uso wa Maria, kwa kiasi fulani Maria akatamani kuurudisha nyuma uso wake lakini akashindwa kutokana na Hidifonce kumvutia kwake zaidi. Maria akashtukia lipsi za Hidifonce zikiwa karibu na lipsi zake.


Mapigo ya moyo yakaanza kumdunda, mzunguko wa damu ukaongezeka mwilini mwake, woga ukaanza kumwingia. Pumzi ambayo ilikuwa ikitoka kwa Hidifoce tayari ilikuwa ikimpata vilivyo. Ghafla akashtukia mikono yake ikishikwa na Hidifonce, Maria akaonekana kulegea kupita kiasi hali iliyomfanya Hidifonce kuanza kumlaza kitandani.


Ghafla kinywa cha Hidifonce kikawa kinywani mwa Maria na kitendo cha kubadilishana mate kuanza mara moja. Kadri muda ulivyokuwa ukizidi kwenda na kitendo kile kuzidi kuchukua nafasi, Maria akajikuta akianza kutoa miguno ambayo alikuwa na uhakika kwamba hakuwahi kuitoa kabla maishani mwake.
Hidifonce akaanza kuipitisha mikono yake mwilini mwa Maria ambaye alihisi vijidudu vikianza kumtembelea mwilini. Maria akaonekana kuchoka pasipo kukimbia, akaonekana kuwa tayari kwa kitu chochote ambacho kilikuwa kikitaka kuchukua nafasi mahali hapo.


Hidifonce akaanza kumchojoa Maria nguo zake. Akaanza na sketi ambayo alikuwa ameivaa, Maria akabaki na skin tight tu. Hidifonce akaanza utundu wake wa kuyachezea mapaja ya Maria ambaye alibaki akilalamika kwa raha. Hidifonce hakutaka kuacha, aliendelea zaidi na zaidi na kuanza kuamia juu.


Blauzi ambayo alikuwa ameivaa ikaanza kufunguliwa vifungo, nguo yake ya ndani ambayo ilikuwa imeyaziba matiti yake ndio ambayo ilikuwa imebakia. Hidifonce akaanza kuipandisha nguo nguo ile, tumbo laini lililokuwa linavutia lilikuwa linaonekana vizuri.


Hidifonce akaanza utundu wake katika tumbo hilo mpaka akakisifikia kitov na kuanza kukichezea alivyotaka. Kelele za mahaba zikazidi kusikika kutoka kwa Maria, muda wote alikuwa akikunja kunja vidole vyake vya miguuni huku akilivuta vuta shuka lililokuwa limetandikwa.


Katika kipindi hicho hakukumbuka kama alikuwa mwanakwaya kanisani kwao wala kukumbuka kama alikuwa mtoto wa mchungaji. Utundu ambao alikuwa akiufanya Hidifonce mwilini mwake ulionekana kumsahalisha yote ambayo yalikuwa yakimhusu.
Maria akalegea kabisa kana kwamba mtu ambaye alikuwa amepoteza fahamu. 


Hidifonce hakuonekana kuwa na haraka, aliendelea kumchezea Maria alivyotaka. Maria akabakia mtupu hali iliyompelekea nae Hidifonce kuvua nguo zake katika kasi ambayo hata yeye mwenyewe ilikuwa ikimshangaza.
“Niacheeeeeeee.....” Maria alimwambia Hidifonce kwa sauti ya chini iliyojaa mahaba.


“Niacheeeeee” Maria aliendelea kumwambia Hidifonce.
Maria alitaka aachwe lakini matendo yake kitandani hapo hayakumaanisha kabisa juu ya kile ambacho alikuwa akikisema. Alikuwa akimvutia Hidifonce kwake zaidi huku akitamani Hidifonce aendelee kufanya kile ambacho alikuwa akikifanya.
“Mamaaaaa...Unaniumi....” Maria alijikuta akipiga kelele mara baada ya kusikia maumivu chini ya kitovu.


Damu zilikuwa zinamtoka na kuanza kuchirizika katika mapaja yake. Akaanza kukuruka na kujaribu kumsukuma Hidifonce lakini Hidifonce hakutaka kutoka. Bado alikuwa akiendelea kupiga pushapu hali ambayo ilimfanya Maria kupiga kelele zaidi.
Ingawa mwanzo alikuwa akimsukuma Hidifonce, ghafla hali ikaonekana kuanza kubadilika, akaanza kumvutia Hidifonce kwake huku akiizungusha mikono yake mgongoni mwa Hidifonce.


Hiyo ndio ilikuwa siku iliyobadilisha kila kitu, hapo ndipo maisha ya Maria yakaonekana kubadilika na kuigia katika mapenzi makubwa na Hidifonce. Akatokea kumpenda Hidifonce kuliko mwanaume yeyote maishani mwake. Maria akawa haambiwi wala hasikii mbele ya Hidifonce. Mara kwa mara alikuwa akivuiwa chupi yake na kufanyiwa mchezo ule ambao ulikuwa ukimbadilisha kupita kiasi.


Umbo lake ambalo lilikuwa likionekana kuvutia likabadilika na kuvutia zaidi. Hipsi zake zikaongezeka na hata tumbo lake kujipanga vilivyo. Maria akaanza maringo, hakujiona kuwa tofauti na wasichana wengine ambao walikuwa wameuanza mchezo ule kitambo. Kila siku alikuwa chumbani kwa Hidifonce huku akimpikia, na kila Hidifonce aliporudi, ngono ilikuwa ikiendelea kama kawaida.

Je, nini kitaendelea?

******************** ************************ ************************* ********************
Simulizi zitakujia hapa hapa kila siku kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa nne asubuhi na ukipitwa na story basi nenda hapo juu kwenye menyu kisha bofya mahali palipo andikwa LOVE & STORY. Pia waweza kudownload Application yetu kwa kubofya neno DOWNLOAD hapo chini ufuate na maelekezo ili uweze kupata story na updates mbalimbali kwa muda muafaka na kwa urahisi zaidi.
 

Tukutane tena kesho muda kama huu.. ahsante


Download

0 comments:

Post a Comment