Pages

Subscribe:

Sunday, April 2, 2017

STORY: SLAVE SEX (MTUMWA WA NGONO) 05

Image result for MTUMWA WA NGONo 01
AGE…(18+)
ILIPOISHIA.
Kitendo cha Magugu kumtizama Gloria moyo wake ukamdunda na kumwenda mbio,ilikuwa ni tofauti na alivyomuona kwenye harusi,Gloria alizidi kuwa mzuri siku hiyo na walivyopeana mikono ya salamu akamtekenya kwenye kiganja chake,na kumkonyeza bila ya Nickson kujua lolote.


SONGA NAYO.

Moyo wa Gloria ulipigwa ganzi ya ghafla hakuelewa ni kitu gani akifanye,Mr.Magugu alizidi kuutekenya mkono wake huku akimkonyeza, alishindwa kuvumilia kwa nguvu zake aliutoa mkono wake mpaka ukamgonga Nickson aliyekuwa...
anaangalia pembeni.
“Vipi Gloria?”


Nickson aliuliza lakini badala ya Gloria kujibu alikaa kimnya,kuna kitu alijifunza lakini hakua ana uhakika nacho.
“Twende Nickson,nataka niwahi leo ofisini,lakini sijakusifia mkeo ni mzuri,huyu ni mchaga vile?”
“Ndio bosi”
“Basi umechagua,kama akihitaji kazi mimi nitamtafutia,asiwe anakaa nyumbani inabidi nayeye achakalike asiwe goalkeeper,kesho na kesho kutwa hautokuwepo,atashindwa pa kuanzia”
“Kweli bosi,utamtafutia kazi?”
“Hilo ondoa shaka”


Kutokana na Elimu ndogo aliyokuwa nayo Gloria kwa Nickson hiyo aliiona ni bahati kwake, hakutegemea kama bosi wake angekuwa mpole kiasi hicho tofauti na siku nyingine zote alizowahi kuishi naye.


Waliingia ndani ya gari na Nickson akampeleka bosi wake mpaka Mbezi beach sehemu anapoishi,wakaagana na Nickson akahaidi kuwa kesho yake atafika ofisini asubuhi na mapema.Kabla ya Nickson kutoka getini Bosi wake alimuita akawa kama ana kitu anataka kumwambia.

“Embu njoo mara moja”
Nickson alitembea kwa adabu.
“Kama nilivyokwambia,mimi ndiye nilifanya mipango ya wewe kupewa nyumba na gari sasa pia nitafanya mipango ya mkeo apate kazi nzuri”
“Lakini hana elimu sana”
“Bwana wee!hapa mjini kwani wanaokaa kwenye maofisi wote wana elimu?hilo swala niachie mimi nilishughulikie”
“Sawa bosi,hata ivyo nashukuru sana Mungu akuzidishie,ahsante kwa kila kitu”
“Anza kumwambia maana naona ni muoga kweli,hata nilivyokuwa namsalimia pale nikawa namshtua shtua akawa anaogopa,mchangamshe bwana”
“Ha ha ha haaa sawa bosi,hilo ondoa shaka bado mgeni wa jiji,atazoea tu”
“Haya usiku mwema kesho uwahi mapema”
“Sawa”
Nickson aliondoka akiwa mwenye furaha moyoni mwake, lakini alipoingia ndani ya gari na kumueleza habari hizo mke wake Gloria ili kuwa ni kinyume, hakuonesha furaha ya aina yoyote ile,jambo ambalo alishindwa kulielewa.


“Sasa mbona hufurahi?”
“Hapana,siwezi kufanya hiyo kazi”
“Sasa kwanini?”
“Basi sijisikii”
“Ngoja nikwambie mke wangu,sina maana mbaya kukuanzisha kazi, hapana,lakini nachotaka mimi uwe unajishughulisha, unajua haya maisha siku yoyote naweza nikatoweka alafu ukawa mzigo kwa watu”
“Nickson naomba twende nyumbani”
Gloria alilengwa na machozi, moyoni alikuwa ana sababu kubwa ya kukataa kazi aliyotaka kupewa na Nickson kupitia mgongo wa Mr.Magugu,alielewa nini maana yake,
kitendo cha kutekenywa mkono wake ndicho kilichomuuma zaidi,kwa kitendo hicho yeye alihesabia ni kama udharirishwaji,alimpenda mme wake na alisikitika sana na kumuonea huruma sababu hakuelewa nini maana ya kazi hiyo.
“Nickson”
Gloria alimuita Mme wake baada ya gari kuwashwa na kuondoka.


“Naam”
“unataka nifanye kazi kweli?”
“Ndio,lakini ukikataa sitakuwa na haja ya kukulazimisha”
“Mimi nipo tayari,lakini sio hiyo ninayotafutiwa na bosi wako”
“Sasa kwanini?yeye ndiye mtu mkubwa hapa mjini atakusaidia kwa kila kitu,na si ajabu ukapata kazi nzuri na ukalipwa vizuri”
“Hujaelewa Nickson wangu”
“Sijaelewa nini?”
“Unajua alinifanya nini pale uwanja wa ndege?”
“Alikufanya nini?”
“Alikuwa akinitekenya mkono wangu,mimi sikupenda na kanikera”
“Aaaah hicho ndicho kinakufanya ukatae kazi yake?iyo kawaida hapa mjini”
“Nickson ndiyo anikonyeze?”
“Kakukonyeza?”
“Ndio”
Hapo Nickson hakua ana haja tena ya kuuliza swali lingine,kwa umri aliokuwa nao alishaelewa nini maana yake,na alivyounganisha matukio alipata jibu kamili kuwa bosi wake kivyovyote anataka kumsogeza karibu mke wake,moyo ulimuuma,

akashusha pumzi nzito iliyochanganyika na wivu ndani yake. Ukimnya ulitawala wa kama sekunde tano.

“Alafu kwanini tusipite tununue vitu vya kupika vya wiki nzima?”
“Sawa”
Nickson hakupinga na kwa bahati nzuri walikuwa wameshafika Buguruni sheli, hapo alikunja kushoto na kunyoosha mpaka Buguruni sokoni,wakanunua vitu vya kupika ndani na kuviweka ndani ya gari.Nickson hakuwa na raha tena, mpaka hapo alikuwa mdogo.


“Gloria”
“Naam mpenzi”
“Nakupenda sana”
“Hata mimi”
“Kweli?”
“Ndio Mme wangu”
Safari ikaendelea na walipofika nyumbani Nickson akajitupa kitandani na kulala chali akitafakari maisha yake ya ndoa na alishaelewa kwa uzuri aliokuwa nao Gloria ni wazi kuwa angekumbana na changamoto nyingi, kama mwanamme ilibidi asimame imara.Akiwa anawaza hayo yote sura ya Mzee Magugu ikamjia kichwani na kujikuta anasonya.


“Baby vipi unawaza nini?”
Gloria aliuliza baada ya kutokeza mlangoni.
“Sio kitu mpenzi”
“Chakula kinakaribia kuiva,tukaoge sasa”
“Poa”
Mchaga Gloria alikuwa ni kama amefundishwa nini maana ya mume, alimpandia Nickson kwa juu kisha kutoa ulimi wake huku akimsogelea mume wake na kuanza kulana denda,sekunde tatu baadaye Nickson akawa amehama kihisia akamtupa Gloria upande wa pili yeye akapanda juu yake huku wakiendelea na mabusu.


“Baby”
“Mhhh”
“Tukaogee bwaaaana,alafu chakula nimeacha jikoni kitaunguaaaa aaaah”
Gloria alitoa sauti ya puani.


“Ahh baby kidogo tu”
“Mimi ni wako,tupo wote,tutafanya baadaye”
“Beebiii,kido….”
Gloria hakuwa na jinsi ya kufanya zaidi ya kumridhisha mme wake na ndiyo mambo aliyofundwa na shangazi zake kipindi anachumbiwa na Nickson,maneno hayakuweza kumtoka,
ilikuwa ni lazima awe tayari muda wowote kwa tendo la ndoa,alivyokumbuka hayo alimrukia Nickson wakaanza kushikana kila sehemu ya miili yao kila mmoja akimvua nguo mwenzake,

mpaka siku hiyo kila mtu alishaelewa ni wapi udhaifu wa mwenzake ulipo.

Ugonjwa wa Gloria ulikuwa sehemu kuu mbili kwenye maziwa na ikulu ndiyo huko Nickson alipocheza napo,hakufanya makosa hata kidogo,dakika tano baadaye wakawa katika tendo la ndoa,baada ya kumaliza hali hiyo wakanyoosha bafuni kuoga kisha kwenda mezani!
“Unaona chakula kimeungua”
“Heee,sasa itakuwaje?”
“Nitapika kingine”
“Hapana,twende tukale nje”
“Nitapika usijali”
Huo ndiyo ulikuwa msimamo wake,Gloria aliingia jikoni na kupika tena, kilivyoiva wakaanza kula mezani,hakuna stori walizopiga nyingine zaidi ya kila mtu kumtamkia mwezake anampenda.


“Hapo umependeza sana”
“Eti eeeh?”
“Ndio Mme wangu,vaa na hiyo tai sasa”
“Tai sipendi sana kuvaa”
“Vaaa kwa ajili yangu”
“Sawa”
Nickson alikuwa amesimama mbele ya kioo kikubwa asubuhi ya saa moja anajiandaa kwenda ofisini kwake, huku Mke wake akiwa bado kitandani anamsifia.
“Ona ulivyopendeza mpaka Napata wivu,huko ofisini hakuna visichana?”
“Hata wakiwepo hawawezi kunitingisha hata kidogo”
“Kweli Mme wangu?”
“Nakwambia ukweli,wacha mimi niwahi basi”
“Chai ipo mezani”
“Hapana, nitachelewa naomba niwahi”
“Okay mpenzi,sogea nikubusu”
Walipigana mabusu na Nickson akatoka nje na kuliendea gari.


Safari ya kwenda ofisini kwake ikaanza,kutokana na msongamano wa magari siku hiyo alichelewa kwa dakika kumi, na alivyofika akaweka gari kando na kushuka.

Wafanyakazi wenzake walivyomuona walifurahi na wengine kumpongeza kwa kurudi kazini tena, baada ya fungate kuisha.

“Alafu bosi kasema ukifika umuone”Alisema sekretari.
“Kwani keshafika?”
“Ndio kaingia sasa hivi, hamjapishana sana”
“Poa wacha niende”
Nickson akanyoosha mpaka ofisini kwa bosi wake,baada ya kugonga alikaribishwa na kuingia.Mzee Magugu alipomuona aliachia tabasamu na kupeana mikono.
“Kahawa?”
“Hapana bosi,niko poa”
“Vipi utokako huko?”
“Huko kwema tu”
“Sasa mkeo alikubali?”
Swali hilo lili mfanya Nickson akae kimnya kwa sekunde kama tano bila kujibu chochote.


“Mimi nataka nikusaidie na nimejitolea huo msaada”
“Bosi,Amesema kwa sasa hivi hayupo tayari”
”Kwanini?”
“Hata nashindwa kuelewa”
“Embu nipatie namba yake ili niweze kufanya naye mazungumzo mimi mwenyewe, kuna kazi tayari nishamtafutia anatakiwa kuanza kesho,nitajie namba zake za simu”
Hakuna siku aliyokuwa katika wakati mgumu kama siku hiyo,Nickson alikuwa akijishauri kichwani ni kitu gani akifanye.


ITAENDELEA...

0 comments:

Post a Comment